Jumla ya madereva 6 wa magari, wamefungiwa leseni zao za udereva, baada ya kubainika kutenda makosa yanayokiuka sheria za usalama barabarani.
Kwa mujibu
wa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi, madereva
hao walibainika kutenda kosa la
kuendesha magari kwa mwendokasi wa Kilomita 116 kwa saa, kwenye maeneo yasiyoruhusiwa, kinyume na sheria za usalama barabarani.
Kamanda Magomi
amebainisha kuwa, hatua hiyo imechukuliwa kupitia operesheni iliyofanyika
katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Juni hadi Agosti, 2026, iliyofanyika kwa lengo la kudhibiti vitendo vya
uhalifu, ikiwemo kuimarisha usalama barabarani.
Kupitia
Operesheni hiyo, kikosi cha usalama barabarani kilibaini jumla ya makosa 5, 291, ya ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani, ambapo kati ya hayo, makossa 4,079, yalihusisha magari na 1, 212, yalihusisha bajaji na pikipiki.
Kamanda
Magomi amebainisha kuwa, wahusika wote walichukuliwa hatua kwa mujibu wa
sheria, ikiwemo kulipa faini za papo kwa papo.
Kufuatia
hali hiyo, Kamanda huyo wa Polisi amewataka madereva na watumiaji wengine wa barabara
kuzingatia sheria za usalama barabarani, ili kuepusha ajali zinazogharimu
maisha ya watu, kusababisha ulemavu wa kudumu pamoja na uharibifu wa mali.

0 Comments