SERIKALI KUTOAMUA RIBA ZA MIKOPO KWENYE BENKI ZA BIASHARA

Serikali imesema haina mamlaka ya kuzipangia benki za biashara viwango vya riba za mikopo, kwa kuwa gharama hizo huamuliwa kwa kuzingatia hali ya soko, mfumuko wa bei, vihatarishi vya mikopo na gharama za uendeshaji.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Mjini, Haidary Sumry, aliyetaka kujua iwapo Serikali inaweza kupunguza riba za mikopo ya biashara ili kuwawezesha wafanyabiashara kulipa madeni kwa wakati.

Luswetula amesema Serikali haiingilii moja kwa moja upangaji wa riba, lakini inaendelea kuchukua hatua za kisera na kiusimamizi kuwezesha wananchi kupata mikopo kwa gharama nafuu.

Amesema Serikali pia imeanzisha mfumo wa Price Comparator, unaowawezesha wakopaji kulinganisha viwango vya riba na gharama za mikopo katika taasisi mbalimbali za fedha, hivyo kufanya maamuzi sahihi na kuongeza ushindani unaoweza kuchangia kupunguza gharama za mikopo.

SOURCE: IPP MEDIA

Post a Comment

0 Comments