Akizungumza na SHINYANGA ONE MEDIA, Mwenyekiti wa kikundi hicho, Husna Mashaka Ally, amesema mkaa huo unapatikana kwenye Duka la Nishati Safi na Salama ya Kupikia wanalolimiliki, lililopo eneo la Bustani ya Kagunze, mtaa Mabambasi, Kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga, ambalo lilizinduliwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Agosti 19, 2026.
Husna amewaomba wananchi wa Shinyanga kukiunga mkono kikundi
hicho kwa kununua na kutumia mkaa huo, hatua ambayo itachangia kuwainua wanawake kiuchumi na kusaidia kupunguza uharibifu wa mazingira, unaotokana
na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa.
Akizungumzia mipango waliyonayo amesema, kikundi hicho kinajiandaa kutembelea shule, vyuo na taasisi nyingine zinazopika chakula kwa wingi, kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati hiyo ili kuongeza idadi ya watumiaji mkoani Shinyanga.
Wanawake na Samia ni kikundi cha wanawake kinachounga mkono ajenda za maendeleo za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ikiwemo juhudi za utunzaji wa mazingira, kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya RAFIKI BRIQUETTES
0 Comments