Idadi hiyo ya vifo imevuka vifo 2,299 vilivyoripotiwa
katika mlipuko wa mwaka 2018–2020, na kuufanya mlipuko wa sasa kuwa mbaya zaidi
kuwahi kutokea nchini humo.
Takwimu hizo zinaonesha pia kuwa visa vipya 101
viligunduliwa ndani ya saa 24 zilizopita, hali inayoendelea kuongeza wasiwasi
kuhusu kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo.
Mlipuko huo unasababishwa na virusi vya Bundibugyo,
aina ya virusi vya Ebola ambayo kwa sasa haina chanjo wala tiba
iliyoidhinishwa.
Mamlaka za afya zinaendelea kuimarisha hatua za kudhibiti
kuenea kwa ugonjwa huo, huku wataalamu wakisisitiza umuhimu wa kugundua
wagonjwa mapema na kuwapatia matibabu kwa wakati.
Source DW

0 Comments