Kwa mujibu
wa Tume ya Uchaguzi ya Zambia, Hichilema amepata kura 1,544,140, sawa na
asilimia 58.87, huku mpinzani wake mkuu, Brian Mundubile, akipata kura
1,030,662.
Mgombea
anapaswa kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura halali ili kushinda katika duru ya
kwanza.
Uchaguzi huo
ulifanyika kwa kiasi kikubwa kwa amani, ingawa upinzani uliripoti vitisho,
ukamataji na matukio ya vurugu.
Zoezi la
kuhesabu kura lilisimamishwa kwa takribani saa sita baada ya maafisa wa
uchaguzi kushambuliwa na kura kuibwa, kabla ya kuanza tena.
Waangalizi
wa kimataifa wamevitaka vyama vya siasa kuepuka kauli za uchochezi na kusubiri
matokeo ya mwisho, yanayotarajiwa kutangazwa Jumatatu.
source DW

0 Comments