PAPA AMTEUA BALOZI VATICAN NCHINI TANZANIA KUWA BALOZI MPYA WA COLOMBIA

Askofu mkuu Angelo Accattino

Baba Mtakatifu Leo XIV tarehe, amemteua Askofu mkuu Angelo Accattino kuwa ni Balozi mpya wa Vatican nchini Colombia.

Kabla ya uteuzi huo, Askofu mkuu  Accattino alikuwa ni Balozi wa Vatican nchini Tanzania.

Askofu mkuu Accattino ambaye ana shahada ya uzamivu katika sheria  za Kanisa, alizaliwa tarehe 31 Julai 1966 nchini Italia.

Baada ya masomo yake ya Kipadre tarehe 25 Juni 1994 akapewa Daraja Takatifu ya Upadre.

Alianza utume wake katika masuala ya diplomasia ya Kanisa, tarehe 1 Julai 1999 ambapo tangu wakati huo, akatekeleza utume wake huko Trinidad na Tobago, Colombia, Perù, Vatican na hatimaye, Marekani na Uturuki.

Baba Mtakatifu Francisko tarehe 12 Septemba 2017 akamteua kuwa Balozi wa Vatican nchini Bolivia na kumpandisha hadhi kuwa ni Askofu mkuu na kuwekwa wakfu kama Askofu mkuu tarehe 25, Novemba 2017.

Tarehe 2 Januari 2023 akateuliwa na Baba Mtakatifu Francisko kuwa Balozi wa Vatican nchini Tanzania na hatimaye, 15 Agosti 2026 Baba Mtakatifu Leo XIV amemteua kuwa Balozi mpya wa Vatican nchini Colombia.

SOURCE: VATICAN NEWS

Post a Comment

0 Comments