Makamu wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, amedondoka ghafla wakati akihutubia Mkutano wa Kitaifa wa kujadili hali ya kisiasa nchini, Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na mustakabali wa Taifa unaofanyika jijini Dar es Salaam.
Jaji Warioba
alikuwa akizungumza katika mkutano huo ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia
Tanzania (TCD), ambapo alikuwa ni mgeni rasmi.
Tukio hilo
limetokea wakati Jaji Warioba akieleza hoja mbalimbali kuhusu hali ya kisiasa
nchini, huku akisisitiza masuala yanayohusu mustakabali wa taifa na umuhimu wa
kujenga mazingira yanayolinda demokrasia.
Baada ya
kuanguka, watu waliokuwa karibu naye walimsaidia na kumtoa ukumbini kwa ajili
ya kupatiwa msaada.
Hata hivy, Mwenyekiti
wa TCD, Dorothy Semu, amewaambia washiriki wa mktanao huo kwamba, hali ya Jaji
Warioba imetengamaa na amekwenda kupumzika.
Mkutano huo
umehudhuriwa na vyama vya siasa kikiwemo Chama Cha Mapinduzi (CCM), Msajili wa
Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa
Tanzania, Juma Ali Khatib, makundi ya uwakilishi wa vijana, wafanyabiashara
pamoja na mabalozi kutoka nchi mbalimbali.
Akizungumza
kabla ya kukutwa na hali hiyo, Jaji Warioba, ameshauri misingi ya usawa,
uadilifu, uwajibikaji na uzalendo, iimarishwe ikiwa ni njia ya kujenga amani ya
kudumu.
Amesema
vyama vya siasa vina wajibu wa kuhakikisha ushindani wa kisiasa haugeuki kuwa
chanzo cha kuwagawa Watanzania.
Kwa upande
wake,Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mtungi amesema ushiriki wa
wadau hao unaonyesha dhamira ya kutafuta muafaka kwa maslahi mapana ya taifa.
Balozi wa Ireland
nchini, Nicola Brennan, amesema uzoefu wa nchi mbalimbali unaonesha kuwa imani
inaweza kujengwa upya na taasisi za kidemokrasia kuimarishwa kupitia mazungumzo
na mageuzi.
Balozi wa
Uswisi nchini, Nicole Providoli, yeye amesisitiza mshikamano wa kitaifa kwamba
unajengwa pale mitazamo tofauti ndani ya jamii inaposikilizwa na kuzingatiwa.

0 Comments