Awali, wakati
akipokea Mwenge kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Peter Masindi, Mkuu wa
Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro, alisema
Mwenge ukiwa katika Wilaya ya Shinyanga utatembelea jumla ya miradi 14 ya
maendeleo.
Alifafanua
zaidi kwamba, kati ya miradi hiyo, saba ipo katika Manispaa ya Shinyanga yenye
thamani ya Sh. bilioni 5.2, huku mingine saba ikiwa katika Halmashauri ya
Wilaya ya Shinyanga yenye thamani ya Sh. bilioni 5.4.
Mtatiro
alibainisha kuwa, Fedha zote zilizotumika kutekeleza miradi hiyo zimeletwa na
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, isipokuwa tu ile michache inayotokana na wawekezaji
binafsi.
Ukiwa katika
Manispaa ya Shinyanga, Mwenge wa Uhuru umekimbizwa umbali wa kilomita 84 na
kufikia miradi mbalimbali, ikiwemo kuzindua mradi wa upanuzi wa mtandao wa maji
katika Kata ya Kolandoto, uzinduzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mwagala katika
Kata ya Ibadakuli, pamoja na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa mwekezaji
binafsi wa Makindo Royal Hotel uliopo mjini Shinyanga.
Mwenge pia umekagua shughuli za Kikundi cha Vijana cha Mkasa Fashion kilichopo Shinyanga mjini, kuzindua duka la nishati safi ya kupikia la Kikundi cha Wanawake na Samia kilichopo katika Kata ya Ndembezi, kufungua Daraja la Dodoma linalowaunganisha wakazi wa Kata za Ngokolo na Ndembezi, kuzindua vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Sekondari Old Shinyanga pamoja na Klabu ya Wapinga rushwa katika Shule hiyo.














0 Comments