Akizindua tume hiyo Agosti 7 Ikulu Jijini Dar es salaam, Rais Samia amesema uchunguzi
huo unalenga kwenda mbali zaidi ya kazi iliyofanywa na Tume ya Jaji Mohamed
Chande Othman, ambayo ilichunguza mazingira na athari za uvunjifu wa amani ulioandamana
na uchaguzi huo.
Tume mpya inaongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani ya
Tanzania, Shabani Ally Lila. Mbali na majaji wa Tanzania, imejumuisha pia Naibu
Jaji Mkuu wa Namibia Petrus Tileinge Damaseb na Jaji wa Mahakama ya Rufani ya
Uganda Barishaki Cheborion.
Rais Samia amesema
kuwajumuisha majaji kutoka nchi hizo mbili kunalenga kuipa tume mtazamo mpana
zaidi. Uganda ni mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC, huku Namibia
ikiwa mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC.
"Tume hii inakwenda kuingia kwa undani zaidi kutafuta
nani hasa," Samia amesema, akieleza kuwa uchunguzi unapaswa kubaini waliohusika,
waliochochea na waliotoa fedha kwa ajili ya ghasia.

0 Comments